Friday, September 30, 2016

FABREGAS, MATA WAACHWA HISPANIA.

KOCHA wa timu ya taifa ya Hispania, Julen Lopetegui amewaacha Cesc Fabregas ba Cesar Azpilicueta katika kikosi chake ambacho kinajiandaa kwa ajili ya mechi za kufuzu michuano ya Kombe la Dunia dhidi ya Italia na Albania. Fabregas ambaye ameshindwa kupata nafasi ya moja kwa moja katika kikosi cha kwanza cha Chelsea msimu huu hakujumuishwa pia katika kikosi cha kocha huyo mwezi uliopita. Mchezaji mwenzake wa Cheslea Azpilicueta mwenye umri wa miaka 27, alitajwa katika kikosi cha mwezi uliopita lakini safari hii naye ametemwa. Kwa upande mwingine nahodha Andres Iniesta amerejea katika kikosi hicho huku pia nyota Jose Callejon wa Napoli ambaye yuko katika kiwango kizuri msimu huu akiitwa.

No comments:

Post a Comment