Friday, September 30, 2016

IBRAHIMOVIC ALIKATAA EURO MILIONI 100 ILI AENDE UNITED - WAKALA.

WAKALA wa mshambuliaji wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic, Mino Raiola amedai mteja wake huyo alipewa ofa ya paundi milioni 100 na klabu ambayo hakutaja kuitaja ya China kipindi cha kiangazi.Nyota huyo wa kimataifa wa Sweden alitua Old Trafford akiwa mchezaji huru majira ya kiangazi baada ya mkataba mkataba wake Paris saint-Germain kumalizika. Ibrahimovic anaripotiwa kukunja kitita cha paundi 200,000 kwa wiki Old Trafford, lakini Raiola amedai mteja wake huyo angeweza kupata zaidi kama angeamua kwenda mashariki ya mbali. Akihojiwa Raiola amesema Ibrahimovic ni mchezaji bora kwani alikataa ofa ya euro milioni 100 kutoa China kwasababu alikuwa akihitaji ushindi zaidi kuliko fedha. Raiola aliendelea kudai kuwa siku zote amekuwa mtu mwenye bahati kwani amekuwa akiwawakilisha mabingwa ambao ni Ibrahimovic, Pavel Ndved na Maxwell ambao wamestaafu na sasa Blaise Matuidi na Gigio Donnarumma.

No comments:

Post a Comment