Friday, September 30, 2016

TERRY KUIKOSA SAFARI YA HULL.

KLABU ya Chelsea kwa mara nyingine itamkosa nahodha wake John Terry katika mchezo wao wa ugenini Jumamosi hii dhidi ya Hull City. Beki huyo mkongwe alirejea mazoezini wiki hii lakini alishindwa kukabiliana na athari za majeruhi ya kifundo cha mguu aliyopata wakati wa mchezo dhidi ya Swansea City mapema mwezi huu. Chelsea imepoteza mechi zote mbili ambazo walikuwa bila nahodha wao huyo, huku wakionyesha udhaifu katika safu yao ya ulinzi aktika mechi dhidi ya Liverpool na Arsenal. Akihojiwa kuelekea mchezo huo wa kesho, Conte amesema terry hatakuwepo kwakuwa bado anauguza majeraha ya kifundo cha mguu. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa beki huyo anaweza kurejea uwanjani baada ya mapumziko kupisha mechi za kimataifa.

No comments:

Post a Comment