Tuesday, September 20, 2016

SIMEONE AMMWAGIA SIFA NEYMAR.

MENEJA wa Atletico Madrid, Diego Simeone amemsifia neymar kuelekea mchezo wao dhidi ya Barcelona utakaochezwa kesho. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 amekuwa akisolewa vikali aina ya maisha huku wengine wakienda mbali kwa kumwambia hajitumi akiwa na Brazil wakati alipoonekana akijirusha sehemu mbalimbali wakati wa michuano ya Copa America. Hata hivyo, Neymar aliwajibu wakosoaji hao uwanjani kwa kuiongoza nchi yake kutwaa medali ya dhahabu ya Olimpiki Agosti mwaka huu. Akihojiwa kuhusiana na Neymar, Simeone amesema nyota huyo ni aina ya wachezaji ambao anawapenda kwani aina ya uchezaji wake ni wa kipekee. Neymar ni mmoja ya wachezaji wanaopewa nafasi ya kutwaa tuzo ya Ballon d’Or sambamba na Lionel Messi, Cristiano Ronaldo na Antoine Griezmann.

No comments:

Post a Comment