Tuesday, October 25, 2016

GRIEZMANN ATWAA TUZO YA MCHEZAJI BORA WA LA LIGA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Atletico Madrid, Antoine Griezmann ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa La Liga msimu uliopita. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa alitangazwa mshindi katika sherehe hizo zilizoandaliwa na viongozi wa ligi hiyo huko Valencia jana, iangawa mweneywe hakuwepo eneo la tukio. Klabu hiyo pia ilishuhudia meneja wake Diego Simeone akitwaa tuzo ya kocha bora wa msimu, beki bora akiwa Diego Godin na kipa bora Jan Oblak. Nyota wa Barcelona alishaguliwa kuwa mshambuliaji bora wa msimu huku Luka Modric wa Real Madrid akitwaa tuzo ya kiungo bora. Msimu uliopita Barcelona walitwaa taji la La Liga wakifuatiwa na Real Madrid nafasi ya pili na Atletico Madrid nafasi ya tatu.

No comments:

Post a Comment