Tuesday, October 25, 2016

PSG WALIKUWA TAYARI KUTOA PAUNDI MILIONI 170 KWA NEYMAR.

KLABU ya Paris Saint-Germain-PSG walikuwa tayari kutoa kitita cha paundi milioni 170 kwa ajili ya kumng’oa Neymar Barcelona majira ya kiangazi, lakini wwalikataa kulipa deni la paundi milioni 40 la nyota huyo wa kimataifa wa Brazil. Nyota huyo amekuwa akiandamwa na kesi za kukwepa kodi toka ahamie Barcelona na kushuhudia baadhi ya thamani na mali zake zikizuiwa na mamlaka husika. Inadaiwa kuwa Neymar alikuwa akitaka mshahara wa paundi milioni 22 kwa mwaka lakini pia pia aliwataka mabingwa hao wa Ufaransa kumlipia deni lake kama kweli wanataka aende Parc des Princes. Kufuatia PSG kukataa suala hilo, Neymar aliamua kusaini mkataba wa miaka mitano zaidi na Barcelona.

No comments:

Post a Comment