Tuesday, October 25, 2016

ARSENAL YAJIPANGA KUMBAKISHA WENGER.

KLABU ya Arsenal bado ina matumaini meneja wake Arsene Wenger ataendelea kuinoa timu hiyo baada ya kumalizika kwa msimu huu lakini wakaongeza kuwa hakuna haraka yeyote ya mazungumzo ya mkataba mpya. Meneja huyo mwenye umri wa miaka 67, anasheherekea miaka 20 ya kuinoa klabu hiyo lakini mkataba wa Mfaransa huyo unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu. Akihojiwa kuhusiana na mustakabali wa meneja huyo, mwenyekiti wa Arsenal Chips Keswick amesema kila mtu anafahamu mchango mkubwa aliotoa kocha huyo katika kipindi cha miaka 20 hivyo wana imani na uwezo wake wa kuwapeleka mbele. Mwenyekiti huyo aliendelea kudai kuwa watakaa na kuzungumza kuhusu mkataba mpya pindi wakati utakapofika. Arsenal inatarajiwa kuikaribisha klabu ya ligi daraja la pili ya Reading katika mzunguko wa nne wa michuano ya Kombe la Ligi baadae leo.

No comments:

Post a Comment