Tuesday, October 25, 2016

PEDRO AKIRI KUFANYA MAZUNGUMZO NA BARCELONA.

MSHAMBULIAJI wa Chelsea Pedro amebainisha kufanya mazungumzo ya kurejea Camp Noun a rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu majira ya kiangazi. Barcelona walikuwa wakitaka kuongeza nguvu katika safu yao ya ushambuliaji na waliona Pedro kama mchezaji anayefaa kwa nafasi hiyo kutokana na mafanikio yake kipindi cha nyuma. Hata hivyo, dili hilo halikufanikiwa na badala yake Barcelona walimsajili Paco Alcacer kutoka Valencia. Akihojiwa kuhusiana na hilo, Pedro alikiri kuzungumza na Bartomeu lakini mazungumzo hayo hayakufikia mbali sana baada ya klabu hiyo kupata chaguo lingine. Hata hivyo, Pedro aliendelea kudai kuwa kwasasa anafurahia maisha yake Chelsea kwani anapata muda wa kucheza jambo ambalo ndio lililomfanya kuondoka Barcelona.

No comments:

Post a Comment