Tuesday, October 25, 2016

SINA TATIZO NA MOURINHO - DE BRUYNE.

KIUNGO mahiri wa Manchester City, Kevin De Bruyne amesema hana tatizo lolote na Jose Mourinho katika kipindi ambacho alicheza chini ya Mreno huyo akiwa Chelsea. De Bruyne alishindwa kupata nafasi katika kikosi cha kwanza akiwa Chelsea na kuamua kuamua kumuuza nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji kwenda Wolfsburg. Mourinho alidai kuwa kiungo huyo hana uwezo wa kupambania nafasi yake katika kikosi cha kwanza, ingawa De Bruyne alikosoa madai ya meneja huyo kwa kuonesha uwezo mkubwa akiwa na Bundesliga na City. Akihojiwa De Bruyne amesema hana tatizo lolote na Mourinho, pamoja na kuwa ameshamuonyesha kuwa yote aliyosema kuhusu yeye yalikuwa sio sahihi.

No comments:

Post a Comment