Monday, October 17, 2016

KAULI KUMPONZA MOURINHO

CHAMA cha Soka cha Uingereza-FA kinafanya uchunguzi kuhusiana na kauli aliyotoa meneja wa Manchester United Jose Mourinho kuelekea mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Liverpool baadae leo. Mourinho alikaririwa akidai kuwa mwamuzi Anthony Taylor ambaye ni mwenye wa Manchester, hataweza kuchezesha vyema pambano hilo kutokana na uteuzi wake kukosolewa. Taratibu za FA huwa hazitaki makocha kujadili suala lolote kuhusiana na mwamuzi kabla ya mchezo. FA inataka kuchunguza matamshi hayo kabla ya kuamua ni hatua gani kama ipo inaweza kuchukuliwa.

No comments:

Post a Comment