Monday, October 17, 2016

DROGBA AGOMA KUCHEZA.

MENEJA wa klabu ya Montreal Impact, Mauro Biello amedai kuwa nyota wao Didier Drogba aligoma kucheza baada ya kuambiwa kuwa hataweza kuanza katika mchezo dhidi ya Toronto. Mshambuliaji huyo wa zamani wa Chelsea mwenye umri wa miaka 38, hakuonekana kabisa katika Uwanja wa Saputo ambapo Impact walipata sare ya mabao 2-2 na kupenya kwenye hatua ya mtoano ya Ligi Kuu ya Soka ya Marekani-MLS. Mapema klabu hiyo ilitoa taarifa kuwa Drogba alienguliwa katika kikosi kufuatia kusumbuliwa na majeruhi ya mgongo. Lakini baada ya mchezo huo, Biello amesema Drogba hakuwepo kwasababu hakutaka kuanzia katika benchi kwenye mchezo huo. Drogba ambaye aliondoka Chelsea Julai mwaka 2015, amekuwa akitumika kama mchezaji wa akiba mara mbili katika mechi nne zilizopita za Impact.

No comments:

Post a Comment