Monday, October 17, 2016

NEYMAR KUSAINI MKATABA MPYA IJUMAA.

KLABU ya Barcelona imethibitisha kuwa mshambuliaji wake nyota Neymar anatarajia kusaini mkataba mpya Ijumaa hii. Barcelona walitangaza taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Brazil ataisaini mkataba mpya ambao utamuweka klabuni hapo mpaka mwaka 2021. Neymar amekuwa akihusishwa na tetesi kuwindwa vilabu kadhaa ikiwemo Paris Saint-Germain lakini sasa mshambuliaji huyo anajipanga kusaini mkataba mpya wa muda mrefu Camp Nou. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 amekuwa katika kiwango bora msimu huu akiwa amefunga mabao manne katika mechi sita za La Liga alizocheza. Neymar alijiunga na Barcelona akitokea Santos mwaka 2013 na ameshinda mataji mawili ya la Liga na moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment