Monday, October 17, 2016

KUFA NA KUPONA ANFIELD LEO.

MACHO na masikio ya wapenzi wa soka duniani baadae leo watakuwa luningani kushuhudia mchezo wa Ligi Kuu ambao utazikutanisa timu mahasimu Liverpool dhidi ya Manchester United. Mchezo huo utakaofanyika Anfield unakutanisha timu hizo zenye uhasimu wa kipindi kirefu nchini Uingereza ambapo klabu hizo kwa pamoja wametwaa jumla ya mataji 87, Liverpool 44 na United mataji 43. Liverpool inakwenda katika mchezo huo ikiwa katika kiwango kizuri kwa kushinda mechi zake zote nne zilizopita za ligi huku United wao wakiwa tayari wameshapoteza mechi mbili msimu huu na wako nyuma ya vinata Manchester City kwa alama tano. Hata hivyo, rekodi ya United wakikutana na Liverpool iko juu ambapo wameshinda mechi nne za ligi zilizowakutanisha huku mara ya mwisho ikiwa ni Januari mwaka huu wakati waliposhinda bao 1-0. Liverpool mara ya mwisho kuishinda United katika Uwanja wa Anfield ilikuwa katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa Europa League msimu uliopita ambapo walishinda mabao 2-0.

No comments:

Post a Comment