Tuesday, October 18, 2016

MODRIC ASAINI MKATABA MPYA MADRID.

KLABU ya Real Madrid imetangaza kumsainisha mkataba mpya Luka Modric ambao utamuweka Santiago Bernabeu mpaka Juni mwaka 2020.  Mkataba wa sasa wa nyota huyo wa kimataifa wa Croatia ulikuwa unamalizika mwaka 2018, lakini sasa amekubali kusaini miaka miwili zaidi. Modric alijiunga na mabingwa wa Ulaya akitokea Tottenham Hotspurs Agosti mwaka 2012 na toka wakati ameimarika na kuwa mchezaji wa kutegemewa Madrid. Kiungo huyo mwneye umri wa miaka 31 ameichezea Madrid mechi 18o za mashindano yote mpaka sasa na kufanikiwa kutwaa mataji mawili ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, mawili ya Super Cup ya UEFA, Kombe la Mfalme, Klabu Bingwa ya Dunia na Supercopa de Espana.

No comments:

Post a Comment