Tuesday, October 18, 2016

LEICESTER WAKOMALIA CHAMPIONS LEAGUE.


MENEJA wa Leicester City, Claudio Ranieri amesema timu yake imetoa kipaumbele kwa michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwasababu wana kipindi kirefu cha kuimarisha kiwango chao katika Ligi Kuu. Leicester watakuwa wenyeji wa FC Copenhagen katika Uwanja wa King Power baadae leo, huku wakiwa tayari wameshinda mechi zao mbili za kwanza za kundi G. Lakini mabinga hao wa Ligi Kuu wameambulia alama nane pekee katika mechi zao nane za ligi msimu huu. Akihojiwa Ranieri amesema katika Ligi Kuu watakuwa salama ifikapo mwishoni mwa mwaka ila kwasasa nguvu zao zipo katika Ligi ya Mabingwa. Leicester wlianza michuano hiyo kwa kuilaza Club Brugge kwa mabao 3-0 kabla ya kuja kupata ushindi wa bao 1-0 kwa Porto.

No comments:

Post a Comment