Tuesday, October 18, 2016

TAJIRI WA MAREKANI AINUNUA MARSEILLE.

MFANYABIASHARA tajiri wa Marekani, Frank McCourt amefanikiwa kuinunua klabu ya Olympique Marseille ya Ufaransa kwa kitita cha euro milioni 45. McCourt ambaye anamiliki Los Angeles Dodgers, amepanga kuwekeza kiasi cha euro milioni 200 katika klabu hiyo kwa kipindi cha miaka minne. Marseille mabingwa wa Ligue 1 mara tisa, ambao walimaliza katika nafasi ya 13 msimu uliopita, kwasasa wanashikilia nafasi ya 12 katika msimamo baada ya kucheza mechi nane. Akihojiwa McCourt mwenye umri wa miaka 63, amesema anataka kufungua ukurasa mpya katika klabu hiyo yenye historia kubwa na kuirejesha njia ya mafanikio.

No comments:

Post a Comment