Thursday, October 27, 2016

ROBO FAINALI EFL CUP: MAN UNITED VS WEST HAM, SOUTHAMPTON VS ARSENAL.

KLABU ya Manchester United wamepangiwa kucheza na West Ham United katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la Ligi baada ya kuwang’oa mahasimu wao Manchester City. United iliitandika City bao 1-0 katika Uwanja wa Old Trafford, bao pekee ambalo lilifungwa na Juan Mata wakati West Ham wao walitinga hatua hiyo baada ya kuwang’oa Chelsea kwa mabao 2-1 katika Uwanja wa London. Katika robo fainali nyingine, Hull City wataikaribisha Newcastke United, Liverpool itapambana na Leeds United wakati Southampton wao wakiwa wenyeji wa Arsenal. Mechi hizo zinatarajiwa kuchezwa kati ya Novemba 29 na 30 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment