Thursday, October 27, 2016

KOMPANY ALIKUWA KACHOKA - GUARDIOLA.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amesema alimtoa nahodha Vincent Kompany wakati wa mapumziko katika mchezo wa Kombe la Lidi dhidi ya Manchester United, kwasababu beki huyo alikuwa amechoka. Kompany mwenye umri wa miaka 30, amekuwa akisumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara hivi karibuni lakini alianza vyema katika mchezo huo wa jana bada ya kucheza kwa dakika 78 katika sare ya 1-1 waliyopata dhidi ya Southampton Jumapili iliyopita. Beki huyo alibadilishana na Aleksandar Kolarov wakati wa mapumziko katika mchezo huo wa Old Trafford huku Guardiola akidai kuwa alichoka na asingeweza kucheza kipindi cha pili. Guardiola pia aliamuacha nahodha huyo katika mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya waliofungwa mabao 4-0 na Barcelona na baada ya hapo akifafanua kuwa alimuacha kwsababu hakuwa fiti.

No comments:

Post a Comment