Thursday, October 27, 2016

NINGEWEZA KUJIUNGA NA NA WEST HAM - IWOBI.

WINGA mahiri wa Arsenal, Alex Iwobi amebainisha kuwa angeweza kujiunga na West Ham United kabla ya kuamua kutua Emirates. Nyota huyo wa kimataifa wa Nigeria, aliibuka katika kikosi cha kwanza cha Arsenal msimu uliopita na toka wakati huo amekuwa mara kwa mara katika kikosi cha kwanza cha meneja Arsene Wenger. Hata hivyo, Iwobi amekiri kuwa pia aliwahi kufanya mazoezi na West Ham kabla ya kuamua kujiunga na klabu kubwa ya Arsenal. Akihojiwa Iwobi amesema Arsenal na West Ham zote zilikuwa zikimuhitaji, hivuo alifanya mazoezini katika klabu zote mbili kwa miaka mitatu, kwasababu huwa wanatafutwa wakiwa na na miaka sita na hawawezi kusajiliwa mpaka wafikishe miaka tisa. Iwobi aliendelea kudai kuwa aliamua kujiunga na Arsenal kwasababu alikuwa akiwashabikiwa toka nyuma na mara zote alikuwa akiiona ni klabu kubwa.

No comments:

Post a Comment