Thursday, October 27, 2016

MDOMO WA MOURINHO WAMUINGIZA MATATANI TENA.

CHAMA cha Soka cha Uingereza-FA kimemfungulia mashitaka meneja wa Manchester United Jose Mourinho kwa kudai kuwa itakuwa vigumu kwa mwamuzi Anthony Taylor kufanya kazi yake kwenye mchezo wao dhidi ya Liverpool. Mourinho aliongeza kuwa kuchaguliwa kwa Taylor kwa ajili ya kuchezesha mechi hiyo ya Octoba 17 kumeongeza shinikizo kwa waamuzi wanaotoka jiji la Manchester. Sheria za FA zinakataza makocha kuzungumzia waamuzi ambao wanachezesha mechi zao. Mourinho amepewa mpaka Octoba 31 awe amejibu mashitaka hayo yanayomkabili.

No comments:

Post a Comment