Thursday, October 27, 2016

SABA WAKAMATWA KWA VURUGU MECHI YA WEST HAM NA CHELSEA.

POLISI jijini London limekamata watu saba kufuatia vurugu zilizozuka wakati wa mchezo wa Kombe la Ligi kati ya West Ham United na Chelsea jana. Chupa za plastiki, viti na sarafu vilikuwa vikirushwa wakati wa mchezo huo ambao West Ham walioshinda mabao 2-1 katika Uwanja wa London, kufuatia mashabiki kugombana mpaka kupelekea polisi kuingilia kati vurugu hizo. Hiyo ni mara ya pili kwa vurugu kuzuka katika uwanja huo mpya wa West Ham msimu huu. Meneja wa West Ham Slaven Bilic amechukizwa na tabi hiyo ya iliyoonyeshwa na mashabiki na kudai kuwa haikubaliki katika soka la sasa.

No comments:

Post a Comment