Thursday, October 27, 2016

HAKUNA UHASAMA BAINA YANGU NA MESSI - RONALDO.

MSHAMBULIAJI nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amepuuza taarifa kuwa kuna uhasama baina yake na Lionel Messi, akisisitiza kuwa wanaheshimiana pamoja na kwamba sio marafiki wa karibu. Wawili hao wamekuwa wakitawala tuzo za Ballon d’Or katika kipindi cha miaka nane iliyopita na wamekuwa wakitajwa kama moja ya wachezaji bora kabisa kuwahi kutokea. Kumekuwa na mijadala mingi inayoendelea kuhusu ni nani bora haswa kati ya wawili hao, lakini Ronaldo amesema hakuna chuki yeyote baina yao. Akihojiwa Ronaldo amesema kumekuwa na hali ya kuheshimiana baina yake ya Messi, na hakuna uhasama wowote kama vyombo vya habari vinavyosambaza.

No comments:

Post a Comment