Friday, October 28, 2016

PLUIJM AREJEA YANGA.

HATIMAYE klabu ya Yanga imefanikiwa kumrejesha kocha wake Hans Van De Pluijm ambaye alijizulu nafasi yake hiyo mapema wiki hii. Kocha huyo alifikia hatua ya kujiuzulu kwa madai kuwa uongozi wa klabu ulikuwa ukifanya mambo bila kumshirikisha zikiwemo taarifa kuwa walikuwa wakipanga kuvunja benchi lote la ufundi. Taarifa za kuvunjwa kwa benchi la ufundi zilisambaa kufuatia ujio wa kocha wa timu ya Zesco United ya Zambia. Hata hivyo, baada ya vikao kadhaa ambavyo vilikuwa vikiongozwa na Waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Nchemba hatimaye klabu hiyo imefanikiwa kumshawishi kocha huyo kuendelea na kibarua chake. Taarifa za kurejea kwa Pluijm zilithibitishwa na viongozi wa Yanga wenyewe pamoja na Waziri Mwigulu.

No comments:

Post a Comment