Friday, October 28, 2016

BARCELONA WAMSHITAKI RAIS WA LA LIGA.

KLABU ya Barcelona imemshitaki rais wa La Liga Javier Tebas kwa mahakama ya juu ya michezo nchini Hispania baada ya kuhoji tabi za wachezaji wao wakati wa mchezo walioshinda mabao 3-2 dhidi ya Valencia. Valencia litozwa faini ya euro 1,500 baada ya chupa za plastiki kurushwa kutoka katika majukwaa kwenda kwa wachezaji uwanjani. Lakini kamati ya nidhamu ya La Liga pia ilikosoa tabia iliyoonyeshwa na wachezaji wa Barcelona wakati wakishangilia bao lao la ushindi. Akihojiwa Tebas amesema suala la kutupa chupa lilipaswa kuchukuliwa hatua lakini baadhi ya wachezaji wa Barcelona nao walionyesha tabia zisizopendeza zilizowakwaza mashabiki wa Valencia. Rais wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu, amesema kauli hiyo ya Tebas inaonyesha jinsi gani asivyowajibika kutokana na wadhifa alionao.

No comments:

Post a Comment