Friday, October 28, 2016

PULIS AONGEZA MKATABA WEST BROM.

MENEJA wa West Bromwich Albion, Tony Pulis amesaini mkataba wa mwaka mmoja zaidi ambao utamuweka katika klabu hiyo mpaka mwishoni mwa msimu ujao. Katika taarifa yake, klabu hiyo imedai kuwa mkataba huo utaleta uhakika na mlinganyo baada ya kununuliwa na mfanyabiashara Guochuan Lai wa China kwenye lengo ya kuimarisha zaidi timu hiyo. Pulis alitua katika klabu hiyo Januari mwaka 2015 wakati wakiwa nje ya eneo la kushuka daraja na kufanikiwa kuipandisha mpaka kumaliza katika nafasi ya 13 na 14 katika Ligi Kuu. Akihojiwa Pulis amesema huu ni wakati wa mabadiliko makubwa kwa klabu hiyo na wakati hilo likitokea inahitaji muendelezo.

No comments:

Post a Comment