Friday, October 28, 2016

MKHITARYAN AAPA KUPIGANIA NAFASI OLD TRAFFORD.

KIUNGO wa Manchester United, Henrikh Mkhitaryan ameapa kupigania nafasi katika kikosi cha kwanza pamoja na kutopangwa katika klabu yake hiyo mpya kwa wiki sita. Nyota huyo wa kimataifa wa Armenia alitua Old Trafford akitokea Borussia Dortmund majira ya kiangazi mwaka huu lakini hajaichezea United toka mechi yao ya Derby dhidi ya Manchester City Septemba 10. Mkhitaryan alipata majeruhi madogo ya msuli wakati wa mapumziko kupisha mechi za kimataifa Septemba, ingawa anadaiwa kuwa tayari alishapona majeruhi hayo kipindi kirefu. Lakini pamoja na kukosa nafasi ya kuchza, kiungo huyo amedai kuwa kamwe hawezi kukata tamaa ya kupambania nafasi yake katika kikosi cha Jose Mourinho.

No comments:

Post a Comment