Friday, October 28, 2016

BABA YAKE NEYMAR ADAI KILICHOMPELEKA MWANAE BARCELONA NI MESSI.

BABA yake Neymar amesema Lionel Messi ndio sababu ya mwanae kuwepo Barcelona na kuthibitisha kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Argentina ndio anayemhusudu. Neymar alijiunga na Barcelona akitokea Santos kiangazi mwaka 2013, na haraka akafanikiwa kutengeneza ushirikiano mzuri na Messi uliosaidia klabu hiyo ya Catalan kutwaa mataji mawili ya La Liga, moja na Ligi ya Mabingwa Ulaya na moja la Klabu Bingwa ya Dunia. Kufuatia Neymar kusaini mkataba mpya utakaomuweka Camp Nou mpaka mwaka 2021, Baba yake amesema kikubwa kilichochangia hilo ni kuwepo kwa Messi katika klabu hiyo. Mzee huyo amesema kijana wake Neymar siku zote amekuwa akimhusudu Messi na ndoto zake kubwa ni kucheza sambamba naye ndio maana yupo Barcelona.

No comments:

Post a Comment