Friday, October 28, 2016

PEREZ NJE WIKI NNE.

MSHAMBULIAJI wa Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha kuwa mshambuliaji wao Lucas Perez anatarajiwa kukaa nje ya uwanja kwa wiki nane baada ya kuumia goti. Perez ambaye alijiunga na klabu hiyo akitokea Deportivo La Coruna Agosti mwaka huu alipata majeruhi hayo kufuatia kukwatuliwa na Denzell Gravenberch wa Reading katika kipindi cha pili cha mchezo wa Kombe la Ligi Jumanne iliyopita. Akihojiwa kuelekea katika mchezo wao wa kesho dhidi ya Sunderland, Wenger alithibitisha taarifa hizo na kudai kuwa watamkosa Perez kwa wiki kati ya sita mpaka nane. Pamoja na kumkosa Perez lakini Arsenal wamepata ahueni kufuatia taarifaz a kurejea kwa kiungo wake Aaron Ramsey. Wenger amesema Ramsey pamoja na Olivier Giroud wote wanatajiwa kuwepo katika kikosi chake kwa ajili ya mchezo huo wa kesho.

No comments:

Post a Comment