Friday, October 28, 2016

MO BEJAIA NA TP MAZEMBE KATIKA FAINALI YA KOMBE LA SHIRIKISHO.

KLABU ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC inatarajiwa kukwaana na MO Bejaia katika mchezo wa fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho. Fainali hiyo itakayochezwa kwa mikondo miwili, itaanzia katika Uwanja wa Mustafa Tchaker huko Blida kwa mchezo wa mkondo utakaochezwa kesho usiku. Bejaia wao watakuwa wakiwania taji lao la kwanza katika michuano hiyo huku Mazembe wao wakiwa wazoefu wa michuano hiyo kwa kutwaa mataji matano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwemo la mwaka jana, moja la Kombe la Washindi na SuperCup tatu za CAF. Mchezo wa marudiano baina ya timu hizo unatarajiwa kufanyika katika Uwanja wa Mazembe jijini Lubumbashi, Novemba 6 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment