Monday, October 31, 2016

MAN UNITED NA SPURS ZAMNYIMA RAHA WENGER.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema mwezi Novemba ndio utakaompa picha nzuri kama kikosi chake kitaweza kushindania taji la Ligi Kuu msimu huu. Arsenal kwasasa wanashika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi wakipishana na vinara Manchester City kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa, kufuatia ushindi wa mabao 4-1 waliopata dhidi ya Sunderland. Hata hivyo, pamoja na kikosi chake kuonekana kufanya vyema lakini Wenger mwenyewe anadhani mwezi ujao ndio utakuwa kipimo sahihi kwani wanakabiliwa na mechi ngumu ikiwemo ile dhidi ya Tottenham Hotspurs na Manchester United. Akihojiwa Wenger amesema kufuatia mechi ngumu watakazokutana nazo anadhani mwishoni mwa mwezi ujao wanaweza kujua zaidi kuhusu hali yao.

No comments:

Post a Comment