Monday, October 31, 2016

AC MILAN WAMNYATIA SCHWEINSTEIGER.

KLABU ya AC Milan inadaiwa kutaka kumuwania kiungo a Manchester United Bastian Schweinsteiger wakati wa kipindi cha dirisha dogo la usajili Januari mwakani. Nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani ameondolewa kabisa katika kikosi cha United huku taarifa za karibuni zikidai kuwa Jose Mourinho amemuondoa hata katika kikosi cha wachezaji wa akiba. Kufuatia hatua hiyo, sasa kuna uwezekano mkubwa wa kiungo huyo kutaka kuondoka Januari na Milan inaweza kuwa chaguo lake. Schweinsteiger pia amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda kucheza katika Ligi Kuu ya Marekani-MLS huku Los Angeles Galaxy ikitajwa kumuwania.

No comments:

Post a Comment