Monday, October 31, 2016

WALCOTT, CAZORLA KUWAKOSA LUDOGORETS.

WINGA wa Arsenal, Theo Walcott mapema amefanya mazoezi tofauti na wachezaji wenzake wakati wakijiandaa na mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Ludogorets ya Bulgaria. Nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza anatarajiwa kukaa nje katika mchezo huo wa kesho kutokana na majeruhi madogo ya msuli wa paja, akiwa pia amekosa mchezo wa Jumamosi iliyopita ambao Arsenal walishinda kwa mabao 4-1 dhidi ya Sunderland. Hata hivyo, Walcott mwenye umri wa miaka 27 anakaribia kupona majeruhi hayo na anaweza kurejea katika mchezo wao wa derby ya kaskazini mwa London dhidi ya Tottenham Hotspurs Jumapili ijayo. Santi Cazorla na Nacho Monreal nao pia bado wanajiuguza na wanatarajiwa kukosa mchezo huo.

No comments:

Post a Comment