Monday, October 31, 2016

LOEW AONGEZA MKATABA UJERUMANI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ujerumani, Joachim Loew ameongeza mkataba mwingine mpya ambao utamalizika baada ya michuano ya Ulaya mwaka 2020. Chama cha Soka cha Ujerumani-DFB kilithibitihsa taarifa hizo mapema leo kuwa Loew ambaye alianza kuinoa Ujerumani mwaka 2006 amekubali kuongeza mkataba mwingine. Mkataba wa sasa wa kocha huyo ulikuwa unamalizika baada ya michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Urusi mwka 2018. Rais wa DFB, Reinhard Grindel amesema Loew amekubali kuongeza mkataba kwakuwa wana malengo yanayofanana ambapo mojawapo ni kutetea taji lao la Kombe la Dunia nchini Urusi na pia kushinda taji la Ulaya mwaka 2020.

No comments:

Post a Comment