Monday, October 31, 2016

ROBBEN KUREJEA PSV BAADA YA KUPITA MIAKA 14.

WINGA mahiri wa Bayern Munich, Arjen Robben anarejea PSV Eindhoven kwa mara kwanza baada ya kupita miaka 14 wakati timu hizo zitakapokwaana katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kesho. Katika mchezo huo PSV wataikaribisha Bayern katika Uwanja wa Philips, mahali ambapo ndipo alipoibukia Robben. Robben mwenye umri wa mika 32 alionyesha mchezo wa kiwango cha juu katika ushindi wa mabao 3-1 iliyopata Bayern dhidi ya Augsburg, baada ya kufunga na kutoa pasi za mwisho mbili ambazo zilitumiwa vyema na Robert Lewandowski na kuwapata ushindi huo. Winga huyo alijiunga na PSV akiwa na umri wa miaka 18 na kufanikiwa kufunga mabao 21 katika mechi 75 alizoichezea klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment