Monday, October 31, 2016

PEPE KUKAA NJE YA UWANJA WIKI NNE.

BEKI wa Real Madrid, Pepe anaweza kukaa nje ya uwanja kwa kipindi cha mwezi mmoja baada ya kupata majeruhi ya msuli. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno alipata majeruhi na kutolewa nje katika kipindi cha kwanza cha mchezo ambao Madrid walishinda mabao 4-1 dhidi ya Alaves Jumamosi iliyopita. Taarifa kutoka katika mtandao wa klabu hiyo zinadai kuwa baada ya kufanyiwa vipimo zaidi leo, imegundulika kuwa Pepe anaweza kukaa nje kwa muda wa wiki tatu mpaka nne. Pepe mwenye umri wa miaka 33 sasa anatarajiwa kukosa mechi sita ukiwemo mchezo dhidi ya mahasimu wao Atletico Madrid utakaofanyika Novemba 19 mwaka huu.


No comments:

Post a Comment