Tuesday, November 1, 2016

MCHEZO DHIDI YA BARCELONA NI KAMA FAINALI - GUARDIOLA.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amesema mchezo wao wa nyumbani wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Barcelona unapaswa kuchukuliwa kama fainali. City walipoteza mchezo wa kwanza kwa kutandikwa mabao 4-0 huko Hispania na kwasasa wanshika nafasi ya pili katika kundi C. Mshambuliaji Sergio Aguero anategemewa kuanza katika mchezo huo wa baadae leo sambamba na beki wa kulia Pablo Zabaleta. Akihojiwa Guardiola amesema walipoteza alama mbili dhidi ya Celtic hivyo wanapaswa kukusanya alama hizo kwa kuhakikisha wanashinda mchezo wao wa leo. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa kwa upande wa Barcelona unaweza usiwe mchezo muhimu sana lakini kwao ni kama fainali.

No comments:

Post a Comment