Tuesday, November 1, 2016

INTER KUMTENGEA VERRATTI ZAIDI YA MILIONI 50.

KLABU ya Inter Milan inadaiwa kuwa tayari kutenga kitita cha paundi milioni 58 kwa ajili ya kumnasa kiungo wa Paris Saint-Germain Marco Verratti. Taarifa juu ya uwezekano wa kutokuwa na maelewano kati ya Verratti na meneja mpya wa PSG Unai Emery, imezifanya klabu nyingi kubwa Ulaya kuangalia uwezekano wa kumsajili. Juventus, Arsenal na Chelsea ni miongoni mwa vilabu vinavyotajwa kumuwania lakini Inter wanadaiwa kuwa tayari kutoa fedha nyingi ili kushindania saini ya kiungo huyo.Kwasasa Inter wana fedha za kutosha za kutumia baada ya kununuliwa na kampuni ya China majira ya kiangazi na wanaweza kuanza kutumia fedha zao hizo katika usajili wa Januari.

No comments:

Post a Comment