Friday, November 18, 2016

CONTE, HAZARD WATWAA TUZO ZA MWEZI.

MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte ameteuliwa kuwa meneja bora wa Ligi Kuu kwa mwezi Octoba. Meneja huyo wa zamani wa Juventus ametwaa tuzo hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kuiongoza Chelsea kushinda mechi tano mwezi uliopita na kuwafanya kukwea mpaka nafasi ya pili katika msimamo wa ligi. Kwa upande mwingine Winga wa klabu hiyo Eden Hazard yeye alitwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi baada ya kufunga mabao matatu na kusaidia lingine moja. Akihojiwa mara baada ya kupokea tuzo hiyo Hazard amesema watu walisema hapigi sana mashuti hivyo amejirekebisha kwa kujaribu kupiga mashuti na na kufunga wakati akiwa uwanjani.

No comments:

Post a Comment