Friday, November 18, 2016

SOUTHGATE KUFANYIWA USAILI JUMATATU.

CHAMA cha Soka cha Uingereza-FA kinatarajiwa kukutana na Gareth Southgate kwa ajili ya kufanywa usaili wa kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya Uingereza. Southgate alikamilisha mechi zake nne bila kufungwa akiinoa timu hiyo kwa muda baada ya kuondoka kwa Sam Allardyce. Southgate anatarajiwa kukutana na jopo likalosimamiwa na mwenyekiti wa FA Gregg Clarke, Ofisa Mkuu Martin Glenn, Mkurugenzi wa Ufundi Dan Ashworth na wajumbe wengine wawili huru kwenye jopo hilo, Howard Wilkinson na Graeme Le Saux. Mkutano huo unatarajiwa kufanyika huko St George Park huku uamuzi wa mwisho ukitarajiwa kutoka wakati wowote baada ya usaili huo.

No comments:

Post a Comment