Friday, December 30, 2016

FEDHA ZA CHINA ZAMTOA UDENDA CLATTENBURG.

MWAMUZI maarufu kutoka Uingereza Mark Clattenburn amedai yuko tayari kwenda nchini China kwani anataka kujikuza zaidi kwenye kazi yake hiyo. Clattenburg mwenye umri wa miaka 41, alitwaa tuzo ya mwamuzi bora wa dunia wa mwaka ya Global Soccer Jumanne iliyopita baada ya kusimamia vyema mechi za fainali ya Kombe la FA, Ligi ya Mabingwa Ulaya na Euro 2016 katika miezi 12 iliyopita. Wakati China ikijaribu kujijenga katika soka kufuatia kusajili wachezaji nyota hivi karibuni wakiwemo Oscar aliyetoka Chelsea na Carlos Tevez aliyetoka Boca Juniors, Clattenburg amedai atakuwa tayari kwenda kama ofa nzuri ikiwekwa mezani. Akihojiwa Clattenburg amesema China inataka kuendeleza soka lao na kama nafasi ikitokea pamoja na kwamba ana mkataba na Ligi Kuu lakini ataangalia mipango yake ya muda mrefu katika kibarua hicho.

No comments:

Post a Comment