Friday, December 30, 2016

NYOTA WA ZAMALEK AACHWA MISRI.

KOCHA wa timu ya taifa ya Misri, Hector Cuper ameita kikosi chake cha awali cha wachezaji 27 kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika-Afcon inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi Januari 14 mwaka huu huko nchini Gabon. Katika kikosi hicho, mshambuliaji wa Zamalek Basem Morsi ameachwa lakini mshambuliaji wa AS Roma Mohamed Salah ambaye amekuwa nje akisumbuliwa na majeruhi kifundo cha mgu ameitwa. Nyota wa Arsenal, Mohamed Elneny naye ni miongoni mwa wachezaji 11 wanaocheza soka nje ya nchi walioitwa. Wachezaji wanne pekee Essam El-Hadary, Ahmed Elmohamady, Mohamed Abdel-Shafy na Ahmed Fathi ndio wamewahi kuchiriki michuano hiyo kabla. Cuper ana kibarua cha kuchuja kikosi hicho kabla ya kubakiwa na wachezaji 23 wanaohitaji kwa ajili ya michuano hiyo. Misri wamepangwa kundi D sambamba na Ghana, Mali na Uganda na mchezo wao wa ufunguzi unatarajiwa kuwa dhidi ya Mali Januari 17 mwakani.

Egypt squad:

Goalkeepers: Essam El Hadary (Wadi Degla), Ahmed El Shenway (Zamalek), Sherif Ekramy (Al Ahly) , Mohamed Awad (Al Ismaily).

Defenders: Ahmed Elmohamady (Hull City) , Mohamed Abdel-Shafy (Al Ahly Jeddah, Saudi Arabia), Ahmed Fathi (Al Ahly),Karim Hafez (Nice, France) , Hamada Tolba (Al Masry) , Ahmed Hegazy (Al Ahly) , Saad Samir (Al Ahly) , Ahmed Dweidar (Zamalek), Omar Gaber (FC Basel, Switzerland) , Ali Gabr (Zamalek).

Midfielders: Abdallah El-Said (Al Ahly) , Amr Warda (Panetolikos, Greece) , Mohamed Elneny (Arsenal) , Tarek Hamed (Zamalek) , Ibrahim Salah (Zamalek) , Mahmoud Hassan 'Trezeguet' , Mohamed Ibrahim (Zamalek) , Ramadan Sobhi (Stoke City).

Forwards: Ahmed Gomaa (Al Masry) , Mahmoud Abdel-Moneim 'Kahraba' (Ittihad Jeddeh) , Mohamed Salah (AS Roma, Italy) , Ahmed Hassan 'Koka' (Braga, Portugal) , Marwan Mohsen (Al Ahly).

No comments:

Post a Comment