Friday, December 30, 2016

MUSTAFI FITI KUIVAA PALACE.

BEKI wa Arsenal, Shkodran Mustafi amepona majeruhi yake ya msuli wa paja na anatarajiwa kuwepo katika mchezo wa derby ya London dhidi ya Crystal Palace lakini winga Theo Walcott na beki wa kushoto Kieran Gibbs wanatarajiw akukosa mchezo huo wa Ligi Kuu utakaofanyika Emirates. Arsenal ilikuwa imemkosa beki wake huyo na kuwafanya kuyumba katika safu yao ya ulinzi baada ya kupoteza mechi mbili kati ya tatu walizocheza wakati hayupo. Akihojiwa Wenger amesema Mustafi mwenye umri wa miaka 24 amerejea mazoezini kama kawaida na atarejea katika kikosi chake. Kocha mbali na kudai kuwa atawakosa Gibbs anayejiuguza goti na Walcott, pia amedokeza habari njema kwa Danny Welbeck akidai kuwa ameshaanza mazoezi na wakati anaweza kurejea uwanjani.

No comments:

Post a Comment