Tuesday, December 27, 2016

GUARDIOLA AINYOOSHEA MIKONO CHELSEA.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amesema itakuwa vigumu kwa kikosi chake kuwafukuzia vinara wa Ligi Kuu Chelsea katika mbio za ubingwa. City wamekwea mpaka nafasi ya pili katika msimamo wa ligi baada ya kuichapa Hull City kwa mabao 3-0 jana na kuwafanya kuwa nyuma ya Chelsea kwa tofauti ya alama saba. Akihojiwa Guardiola amesema wamecheza mechi saba zaidi ya Chelsea hiyo ndio sababu haswa ni kwanini anaona itakuwa vigumu kuwakuta. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa Liverpool ilikaribia kutwaa taji kipindi cha hivi karibuni kwasababu walikuwa wana mchezaji mmoja pekee kwa wiki na msimu uliopita ilikuwa hivyohivyo kwa Leicester City. Guardiola amesema kuwa msimu huu Chelsea na Liverpool ndio nafasi yao kwasababu hawana majukumu mengi. Liverpool na Chelsea zote zimeshindwa kufuzu kushiriki michuano ya Ulaya msimu huu baada ya kumaliza katika nafasi ya nane na 10 msimu uliopita.

No comments:

Post a Comment