Tuesday, December 27, 2016

FUFA YATUMA RAMBIRAMBI KWA WACHEZAJI NA MASHABIKI WALIOKUFA MAJI.

SHIRIKISHO la Soka la Uganda-FUFA limetuma salamu zake za rambirambi baada ya mashabiki na wachezaji wa timu moja ya soka nchini humo kufariki dunia wakati boti waliyokuwa wakitumia kusafiri kupinduka katika Mto Albert. Polisi wamesema jana watu 30 walikufa maji wakati boti hiyo inayodaiwa kuwa ilibeba watu kupita kiasi kupinduka baada ya kukosa uwiano mzuri katika maji. Boti hiyo ilikuwa imebeba wachezaji na mashabiki wa timu ya kijiji cha Kaweibanda ambao walikuwa wakisafiri kwenda kucheza mechi ya kirafiki katika sikukuu za Christmas katika wilaya ya Hoima. Katika taarifa yake, FUFA ilielezea masikitiko yao kufuatia kupoteza maisha kwa wachezaji na mashabiki wa timu hiyo ya kijiji inayotoka wilaya ya Buliisa.

No comments:

Post a Comment