Tuesday, December 27, 2016

SUSO KUONGEZA MKATABA MILAN.

KIUNGO wa AC Milan, Suso ana uhakika kuwa hakutakuwa na tatizo la yeye kukubali kusaini mkataba mpya na klabu hiyo. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23, ameanza kujiimarisha katika klabu hiyo msimu huu baada ya kupelekwa kwa mkopo Genoa katika msimu wa 2015-2016. Suso alifunga mabao mawili katika sare ya mabao 2-2 dhidi ya mahasimu wao Inter Milan mwezi uliopita na kuonyesha umuhimu wake katika kikosi cha Vincenzo Montella. Suso ameshaanza mazungumzo na makamu wa rais wa Milan Andriano Gallian juu ya kuongeza mkataba wake ambao unamalizika mwaka 2019 na anategemea watafikia makubaliano.

No comments:

Post a Comment