Tuesday, December 27, 2016

BEKI WA BILBAO AFANYIWA UPASUAJI WA KORODANI.

KLABU ya Athletic Bilbao imethibitisha kuwa beki wake Yeray Alvarez amefanyiwa upasuaji kufuatia kugundulika kuwa na saratani ya korodani. Beki huyo chipukizi mwenye umri wa miaka 21 ambaye aliibuka La Liga mwaka jana, alifanyiwa upasuaji kuondoa korodani zilizoathirika katika hospitali ya Cruces mapema leo. Taarifa ya klabu hiyo imedai kuwa upasuaji umekwenda kama ulivyopangwa na Yeray anatarajiwa kuendelea kubakia hospitali kwa saa 24 ili kufuatilia maendeleo yake. Inategemewa kuwa beki huyo ataruhusiwa kurejea nyumbani kesho.

No comments:

Post a Comment