Tuesday, December 27, 2016

MAN CITY YATOA WAWILI KWA MKOPO.

KLABU ya Manchester City imethibitisha kuwa Pablo Maffeo na Angelino wamekamilisha uhamisho wao wa mkopo kwenda Girona. Maffeo mwenye umri wa miaka 19 alicheza mechi 13 kwa klabu hiyo inayoshiriki Ligi daraja la Pili nchini Hispania msimu uliopita na sasa anarejea tena Catalunya mpaka mwishoni mwa msimu huu. Beki wa kulia Angelino ambaye anafikisha umri wa miaka 20 Januari 4 mwakani, anataka kupata uzoefu wa kucheza katika kikosi cha kwanza, uzoefu ambao alipata kidogo katika klabu ya New York City FC msimu uliopita. Katika taarifa yake, City imedai kuwa chipukizi wake hao watakwenda Girona kuanzia Januari mosi na dili hilo la mkopo linatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu.

No comments:

Post a Comment