Tuesday, December 27, 2016

INTER YAMUWANIA LUCAS.

KLABU ya Inter Milan inataka kumsajili kiungo wa Liverpool Lucas Leiva kwa mkopo katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo Januari mwakani. Hakuna makubaliano yeyote yaliafikiwa mpaka sasa lakini Inter wanataka kuimarisha kikosi chao kabla ya Serie A haijaanza tena Januari 8. Lucas mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na Liverpool akitokea Gremio mwaka 2007 na ameichezea nchi yake ya Brazil mechi 24. Kiungo huyo ndio mchezaji aliyeitumikia Liverpool kwa kipindi kirefu kwasasa.

No comments:

Post a Comment