Thursday, December 29, 2016

CONCACAF YADOKEZA UWEZEKANO ZABUNI YA PAMOJA KOMBE LA DUNIA 2026.

RAIS wa Shirikisho la Soka la nchi za Amerika ya Kaskazini na kati-CONCACAF, Victor Montagliani amedokeza uwezekano wa kuwepo kwa maombi ya pamoja kati ya Marekani, Mexico na Canada kwa ajili ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2026. Baada ya Urusi na Qatar kuwa wenyeji wa michuano ya mwaka 2018 na 2022, CONCACAF inapewa nafasi kubwa ya kuwa mwenyeji wa michuano ya mwaka 2026. Ukanda huo haijaandaa michuano ya Kombe la Dunia toka Marekani walipofanya hivyo mwaka 1994. Wakati Marekani inaweza kugombea zabuni hiyo yenyewe kwa mara nyingine, Montagliani amedokeza kuwa kuna uwezekano wa kuandaa kwa pamoja. Hakuna Kombe la Dunia liliandaliwa na nchi zaidi moja toka Japan na Korea Kusini walipofanya hivyo mwaka 2002.

No comments:

Post a Comment