Thursday, December 29, 2016

TEVEZ AKAMILISHA USAJILI WAKE KWENDA CHINA.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Manchester City na Manchester United, Carlos Tevez amekamilisha rasmi usajili wake kwenda klabu ya Shanghai Shenhua ya China. Kocha wa Shanghai Gus Poyet amemsajili mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 32 kutoka Boca Junior lakini hakuna taarifa zaidi zilizotolewa kuhusu mkataba wake. Klabu ya Boca Junior ilimtumia salamu za heri Tevez katika klabu yake hiyo mpya huku wakiongeza kuwa siku zote atakuwa katika mioyo yao. Tevez alifanikiwa kushinda taji la Ligi Kuu akiwa na klabu hizo zote za Manchester. Pia alitwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na United mwaka 2008 kabla ya kujiunga na Juventus mwaka 2013 ambako nako alishinda mataji mawili ya Serie A.

No comments:

Post a Comment